Asidi ni kampaundi ya kikemia yenye uwezo wa kutoa protoni ya hidrojeni (H+) kwa kampaundi nyingine inayoitwa besi na tokeo la mmenyuko huo kuwa chumvi pamoja na maji.
Asidi iliyotumiwa na watu tangu karne nyingi ni siki; asidi ndani yake huitwa asidi asetia (CH3COOH).
Asidi nyingine inayotumiwa na watu wengi ni asidi salfuria (H2SO4) katika betri za magari.