Asenia (arseniki) | |
---|---|
Asenia yenye rangi nyeusi ndani ya madini mengine
| |
Jina la Elementi | Asenia (arseniki) |
Alama | As |
Namba atomia | 33 |
Mfululizo safu | Simetali |
Uzani atomia | 74.9216 |
Valensi | 2, 8, 18, 5 |
Densiti | 1.9 hadi 5.72 kufuatana na alotropia zake |
Ugumu (Mohs) | (({ugumu))} |
Kiwango cha kuyeyuka | 1090 K (817 ° °C) |
Kiwango cha kuchemka | 887 K (614 °C) (mvukemango) |
Asilimia za ganda la dunia | 6 · 10-4 % |
Hali maada | mango |
Mengineyo | Asenia ni tahajia ya KAST, Aseniki ya ILSD, Arseniki penginepo katika mtandao |
Asenia (pia: arseniki, aseniki; kutoka kigiriki αρσενικόν "arsenikon" iliyotaja kampaundi ya elementi) ni nusumetali au metaloidi yenye namba atomia 33 katika mfumo radidia. Uzani atomia ni 74.9216.
Asenia ina tabia ya alotropia kwa hiyo kuna maumbo na rangi mbalimbali. Kuna hasa maumbo yenye rangi za kijivu, nyeusi, njano na kahawia. Asenia ya kijivu ina fuwele na tabia za kimetali. Asenia nyeusi hupatikana kwa umbo hobela kama kioo.
Asenia ni sumu kali kwa binadamu.
Kampaundi za asenia hutumiwa kama madawa katika tiba ya watu lakini pia madawa ya kuua wadudu. Madawa yaliwahu kuleta hasara ya kiafya hata kuua watu.
Asenia ikichanganywa na risasi (metali) (plumbi) husaidia katika kutengenezwa kwa beteri za gari ikiboresha umwagaji wa plumbi kiwandani.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Asenia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |