Buibui-mjeledi
Buibui-mjeledi akionyesha pedipalpi na mijeledi
Buibui-mjeledi akionyesha pedipalpi na mijeledi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Faila: Arthropoda
Nusufaila: Chelicerata
Ngeli: Arachnida
Oda: Amblypygi
Thorell, 1883
Ngazi za chini

Familia 5; spishi 31 katika Afrika:

  • Charinidae Quintero, 1986
    • Charinus
      • C. africanus Hansen, 1921
      • C. abbatei Delle Cave, 1986
      • C. fagei Weygoldt, 1972
      • C. kakum Harms, 2018
      • C. madagascariensis Fage, 1954
      • C. milloti Fage, 1939
      • C. seychellarum Kraepelin, 1898
      • C. socotranus Weygoldt, Pohl & Polak, 2002
  • Charontidae Simon, 1892
  • Paracharontidae
  • Phrynichidae Simon, 1892
    • Damon Koch, 1850
      • D. annulatipes (Wood, 1869)
      • D. brachialis Weygoldt, 1999
      • D. diadema (Simon, 1876)
      • D. gracilis Weygoldt, 1998
      • D. johnstonii (Pocock, 1894)
      • D. longispinatus Weygoldt, 1999
      • D. medius (Herbst, 1797)
      • D. sylviae Prendini, Weygoldt & Wheeler, 2005
      • D. tibialis (Simon, 1876)
      • D. uncinatus Weygoldt, 1999
      • D. variegatus (Perty, 1834)
    • Euphrynichus Weygoldt, 1995
      • E. amanica (Werner, 1936)
      • E. bacillifer (Gerstäcker, 1873)
    • Musicodamon Fage, 1939
      • M. atlanteus Fage, 1939
    • Phrynichodamon Weygoldt, 1996
      • P. scullyi (Purcell, 1902)
    • Phrynichus Karsch, 1879
      • P. brevispinatus Weygoldt, 1998
      • P. deflersi Simon, 1887
      • P. exophthalmus Whittick, 1940
      • P. longespina (Simon, 1936)
      • P. madagascariensis Weygoldt, 1998
      • P. scaber (Gervais, 1844)
      • P. spinitarsus Weygoldt, 1998
    • Xerophrynus Weygoldt, 1996
      • X. machadoi (Fage, 1951)
  • Phrynidae

Buibui-mjeledi (kutoka Kiing. whip spider) ni arithropodi wa oda Amblypygi katika ngeli Arachnida wafananao na buibui wa kawaida. Kama hawa wana miguu minane lakini hawawezi kusokota nyuzi za hariri. Mwili wao una sehemu mbili kama buibui: kefalotoraksi (cephalothorax: kichwa na kidari) na fumbatio zilizoungwa kwa pediseli (pedicel) nyembamba kwa umbo wa mrija. Mgongo wa kefalotoraksi ni ngumu na kwa hivyo huitwa gamba (carapace). Kinyume na buibui kelisera (chelicerae) za buibui-mjeledi ni fupi na pedipalpi ni ndefu zenye gando kama kaa. Pedipalpi hutumika kwa kukamata mawindo na kelisera kwa kuyakatakata. Miguu sita tu hutumika kwa kutembea. Jozi ya kwanza imekuwa miembamba na mirefu sana mpaka zaidi ya mara nne urefu wa mwili (inafanana na mijeledi, asili ya jina lao) na hutumika kama vipapasio. Buibui-mjeledi hula arithropodi wengine.

Spishi za Afrika

Picha

Makala hii kuhusu "Buibui-mjeledi" inatumia neno (au maneno) ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio la kutafsiri neno (au maneno) la asili whip spider kutoka lugha ya Kiingereza. Neno (au maneno) la jaribio ni buibui-mjeledi.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.