Mji Mdogo wa Chalinze
Nchi Tanzania
Mkoa Pwani
Wilaya Chalinze
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 48,000

Chalinze ni jina la mji mdogo ambayo imekuwa makao makuu ya Wilaya ya Chalinze katika Mkoa wa Pwani, Tanzania. Eneo la mji linaundwa na kata za Bwilingu (Chalinze yenyewe) na Pera.

Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata hizo mbili zilikuwa na wakazi wapatao 48,000 walioishi humo. [1]

Chalinze iko km 110 kutoka Dar es Salaam. Inajulikana kama njiapanda muhimu kwenye barabara kuu za Tanzania. A14 ya kwenda Kilimanjaro na Tanga inaachana hapa na A7 ya kuelekea Morogoro - Iringa ikiendelea kama A104 hadi Mbeya - Zambia/Malawi. Kwa madereva ni maarufu kwa sababu polisi wa barabarani hupima mwendokasi wa magari kwa kutumia mitambo na wengi wanalazimika kulipa faini.

Shughuli kuu za kiuchumi katika mji huo ni kilimo cha mazao ya chakula na biashara, pia ufugaji unafanyika kwa kiwango kidogo.

Mji wa Chalinze haujawahi kuandaliwa Mpango wa Jumla kwa ajili ya kusimamia, kuongoza na kudhibiti matumizi ya ardhi ya mji huo kulingana na Sheria ya Mipangomiji namba 8 ya mwaka 2007.

Changamoto zinazokabili Mji wa Chalinze

Mji wa Chalinze, kama ilivyo katika miji mingi nchini, unakabiliwa na changamoto mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kimazingira zinazosababisha mji huo kukua holela. Changamoto hizo ni pamoja na zifuatazo:

Marejeo

  1. Sensa ya 2012, Pwani - Bagamoyo DC. Jalada kutoka ya awali juu ya 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2016-06-10.
Kata za Wilaya ya Chalinze - Mkoa wa Pwani - Tanzania

Bwilingu | Kibindu | Kimange | Kiwangwa | Lugoba | Mandera | Mbwewe | Miono | Mkange | Msata | Msoga | Pera | Talawanda | Ubenazomozi | Vigwaza


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Pwani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Chalinze kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.