"Kristo na Mhalifu" kadiri ya Nikolai Ge.

Dismas Mtakatifu ni jina lisilo na hakika la mhalifu aliyesulubiwa pamoja na mwenzake na Yesu kwa amri ya Ponsyo Pilato.

Habari hii inasimuliwa na Injili zote (Math 27:38; Mk 15:27-28,32; Lk 23:33; Yoh 19:18) lakini ni Luka tu anayesema kuwa, kati ya hao wawili waliokuwa msalabani kandokando ya Yesu, mmoja alitubu na kumuomba kwa imani, "Ee Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako".

Yesu hakuchelewa kumjibu: "Kweli nakuambia, leo hii utakuwa nami katika paradiso".

Ndiyo sababu Wakristo wengi wanamheshimu kama mtakatifu, hasa tarehe 25 Machi[1].

Tazama pia

Tanbihi

  1. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Dismas Mtakatifu
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dismas Mtakatifu kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.