Maandamano ndani ya katakombu la Mt. Kalisti mjini Roma.
Makaburi ndani ya Katakombu la Domitila, Roma.
Katakombu la Paris.
Yesu na Mitume katika katakombu la Domitila, Roma.
Alama Chi-Rho pamoja na Alfa na Omega, Katakombu la Domitila, Roma.

Katakombu (kutoka neno la Kilatini catacombae) ni mahandaki yaliyotengenezwa chini ya ardhi kwa mazishi na kwa malengo ya kidini. Kwa namna ya pekee yanafikiriwa yale ya Dola la Roma.[1]

Makatakombu yote ya Roma yalipatikana nje ya ngome ya mji, kwa sababu haikuruhusiwa kuzika ndani yake,[2] yakiwapa Wakristo waliodhulumiwa na serikali mahali pa kufaa kwa kuheshimu wafiadini wao. Walikuwa wakikutana kusali katika nyumba za watu binafsi, au kwenye katakombu.

Katika mahandaki hayo inapatikana michoro ya ukutani ambayo ni kati ya kazi za kwanza za sanaa ya Kikristo.

Tanbihi

  1. Other examples include a Neolithic long barrow, an Ancient Egyptian necropolis, or modern underground vaults such as the Catacombs of Paris. The word referred originally only to the Roman catacombs, but was extended by 1836 to refer to any subterranean receptacle of the dead. "Catacombs", Online Etymology Dictionary, accessed 10 July 2010.
  2. Hurst, John Fletcher (1897). History of the Christian Church 1. Eaton and Mains. 

Marejeo

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Katakombu