Maabara ya uganga wa kansa huko Taiwan.
Maabara ya biolojia ya molekuli huko Poznan, Poland.
Benchi katika maabara ya kemia.

Maabara (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza: Laboratory) ni jengo au chumba maalumu kinachotumika kwa ajili ya majaribio na utafiti wa kisayansi.

Kuna aina mbalimbali za maabara, mfano: maabara za biolojia, maabara za kemia, maabara za fizikia n.k.

Vilevile kuna maabara zinazotumika katika hospitali na katika majaribio mengine ya kisayansi. Kwa mfano, maabara ya biolojia ni jengo au chumba maalumu kwa ajili ya kufanyia majaribio yahusuyo viumbe hai.

Historia

Maabara za zamani katika nchi ya Uingereza zilikuwa za kutengenezea dawa. Vita vya pili vya dunia vilifanya maabara ziwe kubwa kwa minajili ya kutengenezea zana za vita za kiatomiki.

Leo maabara bado zinatumika kwa madhumuni ya kutengenezea na kujaribu dawa, kuunda zana za vita na pia kufundisha katika shule.

Sheria za maabara

Sifa za maabara

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Maabara kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.