Justitia, ishara ya mahakama. [1] [2]


Mahakama ni mfumo wa wataalamu na kamati maalumu ambao unatafsiri na kutumia sheria katika jina la wananchi, la jamhuri au la mfalme.

Mahakama pia inatoa mfumo wa kutatua migogoro. Chini ya mfumo wa mgawanyo wa madaraka mahakama kwa ujumla haitungi wala haiundi sheria (ambayo ni kazi ya bunge) wala kutekeleza sheria (ambayo ni wajibu wa serikali), bali inatafsiri sheria na kutumia na kutekeleza katika ukweli wa kila kesi.

Mahakama ina kazi ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria kwa watu wote.

Kwa kawaida kuna mahakama za ngazi mbalimbali; mahakama za juu zinapokea rufaa dhidi ya kesi za ngazi za chini hadi mahakama ya rufaa ya mwisho inayoitwa mahakama kuu au mahakama ya katiba. Tawi hili la mahakama lina uwezo wa kubatilisha sheria zisizolingana na katiba ya nchi.

Neno "mahakama" pia hutumika kumaanisha kwa pamoja maafisa ndani yake kama vile majaji, mahakimu na makarani wengine.

Mahakama na sheria

Kimsingi mahakama ina kazi ya kutumia sheria zilizopo na kuamua juu ya matumizi yao. Hali halisi sheria haziwezi kutaja kila kitu kinachoweza kutokea hivyo ni mahakama zinazoamua kwa njia ya kulinganisha kesi, sheria na maazimio ya mahakama yaliyotangulia.

Kwa hiyo mahakama zinashiriki kiasi katika kazi ya kutunga haki hasa pale ambako sheria za bunge zinaacha pengo.

Kidesturi muundo wa haki na sheria katika Uingereza na Marekani unaziachia mahakama nafasi kubwa zaidi kuendeleza taratibu za kisheria.

Tazama pia

Simple English Wiktionary
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno:
mahakama


Masomo zaidi


Maandiko ya Chini

  1. Hamilton, Marci. Mungu dhidi ya Gavel, ukurasa wa 296 (Cambridge University Press 2005): "Ishara ya mfumo wa mahakama, inayonekana katika majengo ya mahakama kote Marekani, ni Bi Justice aliyefungwa macho."
  2. Fabri, Marco. Changamoto ya kubadilisha mifumo ya kimahakama, ukurasa wa 137 (IOS Press 2000): "mfumo wa kimahakama unatarajiwa kuwa wa kisiasa, ishara yake ikiwa Bi Justice aliyefungwa macho akishika mizani."