Tafsiri ni njia mojawapo ya kutunga makala katika Wikipedia ya Kiswahili (swwiki). Mara nyingi tutatumia makala za Wikipedia ya Kiingereza (enwiki) au Simple Wikipedia (simple - inajaribu kutumia Kiingereza chepesi, lakini wakati mwingine wepesi wake ni maelezo ya kitoto tu).

Kabla ya kutafsiri[hariri | hariri chanzo]

Kuna mambo kadhaa tunayohitaji kuyaangalia kabla ya kutafsiri:

Hifadhi katika sehemu yako kwanza[hariri | hariri chanzo]

(Ona: Msaada:Jamii)

Programu za kutafsiri[hariri | hariri chanzo]

Ona pia: Msaada:Tafsiri ya kompyuta

Kabla ya kutumia programu ya kutafsiri:

  • Soma matini ya Kiingereza, tafakari unachotaka kusema kwa Kiswahili
  • Vunja sentensi ndefu za Kiingereza na kuzigawa kwa sentensi kadhaa za Kiswahili, kwa maneno yako. Programu zote zinashindwa kutafsiri sentensi ndefu.
  • Usifuate muundo wa sentensi ya Kiingereza kama ni tofauti na muundo wa Kiswahili. Mara nyingi Kiswahili kinatumia vitenzi ambako lugha za kizungu hutumia nomino pekee.
  • usikubali pendekezo la programu kwa maneno ya Kiingereza ambayo hujui au huna uhakika nayo. Utafute kwanza visawe vya Kiingereza (kwa mfano hapa), tafakari neno lina maana gani katika matini yako halafu utafute neno la Kiswahili.
  • Ujipatie Kamusi za TUKI English-Kiswahili na Kiswahili-English au nyingine. Zinapatikana mara kwa mara kwenye inteneti kwa kupakua kama pdf. Au ujaribu kurasa za kutafsiri tofauti kando-kando, pamoja na google kuna https://sw.glosbe.com.

Google translate

Wikipedia Content Translation