Kazi ya musuli mkononi.

Misuli [1] ni sehemu ya mwili wa wanyama na binadamu inayowezesha mwendo wa viungo vyake. misuli inaundwa na tishu ya pekee yenye uwezo wa kujinywea na kulegea. Wakati wa kujinywea huwa mifupi zaidi. Kwa njia hii misuli inayounganishwa na mifupa ya mkono au mguu huleta mwendo wa viungo hivi.

Aina za musuli:
misulia milia, misuli myororo, misuli ya moyo

Aina za musuli

Misuli hutofautishwa kwa namna mbalimbali:

Mara nyingi hutofautishwa namna tatu za misuli:

Misuli milia

Misuli ya kiunzi na moyo huitwa pia "misuli milia" kutokana na milia inayoonekana usoni mwao. Milia hii inatokana na muundo wa misuli hii inayofanywa na vinyuzi virefu vya rangi mbili vinavyopangwa taratibu katika misuli na kuonyesha milia meupe na mekundu kwa kubadilishana. Vinyuzi vyekundu ni protini za kiaktini na vinyuzi vyeupe ni protini kimiosi.

Muundo wa misuli

Misuli inaundwa na seli za pekee zenye uwezo wa unyweo. inatekeleza unyweo baada ya kupokea kiamshi kupitia neva. Kiamshi ni mshtuko wa umeme unaopitishwa kutoka seli kwenda seli nyingine. Seli za misuli huwa na protini za kiaktini na kimiosini.

Unyweo wa misuli

Wakati misuli inapokea kiamshi kutoka neva nafasi katika utando wake inapitisha kalsi na kalsi inasababisha aina mbili za protini kuingiliana hivyo kufupisha urefu wa misuli.

Jinsi ya kuunda misuli

Marejeo

  1. "Misuli latokana na Kilatini/Kiingereza "musculus"/"muscle". Neno la Kilatini lamaanisha "panya mdogo" kwa sababu wazee walilinganisha umbo la misuli ya kujinywea na umbo la panya mdogo anayejificha chini ya ngozi.

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya anatomia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Musuli kama matumizi yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.