Nyuki
Jike la nyuki-bungu (Xylocopa caffra)
Jike la nyuki-bungu (Xylocopa caffra)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno chembamba sana)
Familia ya juu: Apoidea
(bila tabaka): Anthophila (Nyuki)
Ngazi za chini

Familia 7:

  • Andrenidae Latreille, 1802
  • Apidae Latreille, 1802
  • Colletidae Le Peletier, 1841
  • Halictidae Thomson, 1869
  • Megachilidae Latreille, 1802
  • Melittidae Schenck, 1860
  • Stenotritidae McGinley, 1980
Mwili wa nyuki. A: Kichwa B: Toraksi (kidari) C: Fumbatio. 1: Gena (shavu) 2: Verteksi (paji) 3: Oselli (macho sahili) 4: Papasio 5: Jicho tata 6: Ndevu 7: Kinywa 8: Mguu wa mbele 9: Femuri (paja) 10: Mguu wa kati 11: Ukucha 12: Tarsi 13: Tibia (goko) 14: Mguu wa nyuma 15: Sterno 16: Mwiba 17: Ubawa wa nyumba 18: Ubawa wa mbele

Nyuki ni wadudu wa kundi bila tabaka Anthophila katika familia ya juu Apoidea ya oda Hymenoptera wenye mabawa manne angavu na mwiba nyuma ya mwili wao. Hukusanya mbelewele na mbochi ya maua kama chakula chao.

Spishi inayojulikana hasa ni nyuki-asali (Apis mellifera) ambaye hufugwa kila mahali duniani. Kuna spishi zaidi ya 20,000 zinazojumlishwa na biolojia kati ya nyuki lakini ni wale wa jenasi Apis wanaotengeneza asali inayovunwa kwa matumizi ya binadamu.

Umbo la nyuki

Mwili una pande tatu jinsi ilivyo kwa wadudu wote: kichwa mbele, kidari katikati na tumbo nyuma, halafu jozi tatu za miguu na jozi mbili za mabawa.

Mwili huwa na nywele na rangi kali za njano na nyeusi kama onyo kwa maadui.

Nyuma ya tumbo wanabeba mwiba wanaotumia kudunga endapo wakihisi kuna hatari au wameshambuliwa. Wakidunga mwiba huwa wanaingiza pia kiasi kidogo cha sumu katika kidonda. Sumu hii inasababisha maumivu na watu wengine wanaathiriwa vikali na sumu hii lakini si kila mtu. Kuna nyuki wanaokufa baada ya kudunga mwiba kwa sababu mwiba unabaki kwenye kidonda lakini wengine wanaweza kutoa mwiba na kudunga tena.

Wadudu wa kijamii

Spishi kadhaa za nyuki ni wadudu wa kijamii maana yake wanaishi kwa makundi si peke yao kama aina nyingine za nyuki. Wanajenga sega ya nta ndani ya mzinga wa nyuki na humu wanatunza asali yao.

Kuna aina tatu za nyuki ndani ya kundi hili nao ni:

Picha

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nyuki
Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyuki kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.