Rasi Agulhas (ing. Cape Agulhas) ni mahali pa kusini zaidi pa bara la Afrika. Iko karibu na mji wa Agulhas katika Afrika Kusini. Iko karibu pia na Rasi ya Tumaini Jema iliyo maarufu zaidi.
Ni mpaka kati ya maji za Atlantiki na Bahari Hindi na mstari unaoelekea kusini kutoka hapa umekubaliwa na Shirika la Kimataifa la Hidrografia kuwa mpaka kati ya bahari hizi mbili.