Samaki (pia: Hutu) ni kundinyota ya zodiaki inayojulikana kimataifa kwa jina lake la kimagharibi la Pisces[1]. Ni moja ya makundinyota yanayotambuliwa na Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [2]
Nyota za Samaki huwa haziko pamoja kihalisi lakini zinaonekana tu vile kutoka duniani. Kwa uhalisi kuna umbali mkubwa kati yao, kama ziko mbali au jirani nasi. Kwa hiyo kundinyota "Samaki" inaonyesha eneo la angani jinsi tunavyoiona kutoka Duniani.
Mabaharia Waswahili wamejua nyota hizi kwa jina la Hutu linalotokana na Kiarabu الحوت al-ḥuut ambalo linamaanisha "samaki". Jina hili lilipokelewa na Waarabu kutoka kwa Wagiriki wa Kale waliosema Ιχθύες ikhthies na majina yenye maana hiyohiyo ya "samaki" yalitumiwa pia na mataifa mengi ya kale.
Katika mitholojia ya Wagiriki nyota zake zilionyesha mungu wa kike wa mapenzi Aphrodite pamoja na mwanawe Eros waliokimbia dubwana Typhoni kwa kuruka katika mto Frati na kuchukua umbo la samaki. Ili wasipoteane kwenye maji walifunga kamba kati yao, na hapo asili ya jina la Kiarabu la nyota Alfa Piscium "Al-Risha" linalomaanisha "kamba" maanake kwenye picha iko mahali pa kamba inayounganisha samaki mbili.
Katika unajimu wa kisasa katika Afrika ya Mashariki jina "Hutu" limesahauliwa badala yake tafsiri „samaki“ imekuwa jina la kawaida.
Hutu iko angani kwenye mstari wa Zodiaki kati ya Ndoo (pia DAlu, lat. Aquarius) upande wa magharibi na Kondoo (pia Hamali, lat. Aries) upande wa mashariki.
Nyota angavu zaidi ni
Jina la (Bayer) |
Namba ya Flamsteed |
Jina (Ukia) |
Mwangaza unaoonekana |
Umbali (miakanuru) |
Aina ya spektra |
---|---|---|---|---|---|
η | 99 | Kullat Nunu | 3,62m | 294 | G7 IIIa |
γ | 6 | 3,70m | 131 | G9 III Fe-2 | |
α | 113 | Alrescha | 3,82 | 139 | A0pSiSr + A3m |
ω | 28 | 4,03 | 106 | F4 IV |
![]() |
Makundinyota ya Zodiaki Majina ya kisasa yanafuatwa kwa mabano na jina la mabaharia na jina la Kilatini (la kimataifa) |
![]() |
---|---|---|
Kaa (Saratani – Cancer |