Angela Merichi

Angela Merichi (21 Machi 147427 Januari 1540) alikuwa mtawa nchini Italia.

Ametambuliwa na Kanisa Katoliki kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 27 Januari[1].

Maisha

Angela Merichi alizaliwa eneo liitwalo Desenzano, karibu na mji wa Brescia nchini Italia, tarehe 21 Machi, mwaka 1474.

Alifuata kanuni za Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko, akawakusanya pamoja wasichana, ambao aliwafundisha kutenda matendo ya huruma.

Mwaka 1535, huko Bresha, alianzisha shirika la Waursula, chama cha wanawake waliojishughulisha kuwafundisha wasichana maskini jinsi ya kuwa Wakristo wema.

Alifariki mwaka 1540.

Tazama pia

Tanbihi

  1. Martyrologium Romanum

Marejeo

VIungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.