Denizli ni mji uliopo mwishoni mwa mashariki ya mto Büyük Menderes, ambapo kuna maporomoko ya mita zaidi ya mia, katika kusini-magharibi mwa nchi ya Uturuki, kwenye Mkoa wa Aegean.
Mji una wakazi wapatao 400,000 (kwa sensa ya 2006) na ndiyo mji mkuu wa Jimbo la Denizli katika Majimbo ya Uturuki. Huu ni mji unaokua sana katika sekta ya viwanda.
Mji wa Denizli umepata mafanikio makubwa sana kiuchumi hasa kwa shughuli zake za utengenezaji wa nguo na kuzusafirisha nchi za nje[1].
Mji huu umekuwa kituo kikubwa cha uzalishaji wa bidhaa zinazotazamiwa kupelekwa nchi za nje, Denizli hutajwa mara kwa mara, ukiwa sambamba na miji mingine ya Uturuki, ikiwa kama miji yenye kupiga hatu kubwa sana kimaendeleo[2].
Jina la Denizli linamaana ya "maeneo yenye bahari au ziwa" kwa Kituruki, lakini mji wenyewe haupo katika pwani. Jina linatokana na tahajia kadha wa kadha ambazo zina vyanzo vya maji yanayopita chini kwa chini na kuelekea katika eneo la mkoa wa karibu ya ziwa lililopo karibu na mji huko Uturuki.[3]
Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Denizli kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |