Kikorsika (Corsu au lingua corsa) ni mojawapo ya lugha za Kirumi inayotumika na watu wasiopungua 150,000, hasa katika visiwa vya bahari ya Tireni. Inafanana sana na Kiitalia, hasa lahaja ya mkoa wake wa Toscana[1], kiasi kwamba wengine wanakiona Kikorsika kuwa lahaja, si lugha ya pekee.
Jina linatokana na kisiwa cha Korsika ambapo ilikuwa lugha ya kawaida hadi karne ya 20, ilipozidiwa na Kifaransa kiasi kwamba inaelekea kufa[2]. Kumbe inaendelea vizuri zaidi kaskazini mwa kisiwa jirani, Sardegna (Italia).
![]() |
Wikiversity has learning materials about Kikorsika |
Corsican travel guide kutoka Wikisafiri
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kikorsika kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |