Rafu ya kukausha tambi mjini Seoul (Korea Kusini)
Spaghetti kwenye sahani na supu ya nyanya na jibini juu yake
Supu ya tambi ya Kichina pamoja na nyama ya kuku

Tambi ni chakula kinachotengenezwa kutoka kwa kinyunga cha unga na maji kuwa kama milia membamba inayopikwa katika maji au supu. Ni chakula muhimu katika nchi nyingi hasa Italia, China, Japani na Korea. Siku hizi zimeenea kote duniani. Aina zinazoliwa sana kimataifa ni pasta zenye asili ya Italia hasa spaghetti.

Tambi bichi na tambi kavu

Tambi zinaweza kutengenezwa jikoni na kupikwa zikiwa bichi. Lakini kwa kawaida huandaliwa kiwandani na kuuzwa ilhali zimekauka. Tambi kavu haziozi zinaweza kutunzwa kwa muda mrefu na zinapikwa haraka kwa muda wa dakika 8-15. Wachina waligundua njia za kutengeneza tambi zinazopikwa katika muda wa dakika 3 pekee.

Tambi za nafaka na tambi za wanga nyingine

Aina nyingi za tambi hutengenezwa kwa kutumia unga wa nafaka kama vile ngano au mchele. Kuna pia aina zinazotumia wanga ya maharagwe, soya au viazi.

Tambi za kale kabisa zinazojulikana zimekutwa na wanaakiolojia nchini China kando la Mto Njano. Zina umri wa miaka 4,000 na zilitengenezwa kwa unga ya mtama.

Aina za tambi

Kuna aina nyingi sana za tambi zinazotofautiana kwa umbo, rangi na ladha. Tabia hizi zinategemea na aina ya unga ambayo ni msingi wa tambi lakini pia na nyongeza kama vile mayai, mafuta, jibini na mengine ndani yake.

Aina za kimsingi ni pamoja

Kuna njia mbalimbali za upishi kwa mfano

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Tambi
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tambi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.