Jamhuri ya Kenya |
![]() Makala hii imepangwa kwa mfululizo: |
|
|
Nchi zingine · Atlasi |
Uchaguzi wa rais nchini Kenya ulikuwa na matatizo mengi na kusababisha kipindi cha mvurugo na vifo.
Baada ya Raila Odinga wa ODM kuongoza katika hesabu ya kura kwa muda mrefu Tume ya Uchaguzi ya Kenya lilisimamisha hesabu ya kura kwa muda wa usiku mmoja na baada kuanza upya kura za Mwai Kibaki wa PNU zilikuwa mbele. Tume ikamtangaza Kibaki kuwa mshindi aliyeapishwa mara moja bila kusubiri muda wa kisheria kwa malalamiko. Watazamaji waliona kasoro, makosa na matokeo yaliyodokeza ya kwamba hesabu ya kura ilibadilishwa kwenye ngazi za kupiga jumla za kura kimkoa na kitaifa. Vilevile kuna madokezo ya kwamba kura za kiraisi ziliongezwa katika usiku ambako hesabu ilisimamishwa.
Matokeo yaliyotangazwa ni kama yafuatayo:
Wagombea wengine walimaliza kwa kura chache tu.
Wabunge 207 walichaguliwa. Kura zitarudiwa katika majimbo 3. Wabunge 12 wa ziada watateuliwa na rais. Akifuata kawaida atawateua kufuatana na nguvu ya vyama bungeni.
Magazeti yalitoa taarifa ya kwamba wabunge 30 wa vyama vidogo waliunda "Kundi la vyama vidogo bungeni" (Small Parties Parliamentary Group); idadi hii ingejumlihsa wabunge waliohesabiwa juu kama kundi la PNU.
ODM | NARC ilishirikishwa na ODM |
PNU | Vyama shirikishwa vya PNU |
KANU Chama chirikishwa na PNU |
ODM-Kenya | Wabunge wanaojitegemea | JUMLA | |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Wabunge | 99 | 3 | 43 | 21 | 14 | 16 | 11 | 207(of 210) |
Vyama shirikishwa vya PNU- KANU (14), Sisi Kwa Sisi (2), Safina (5), NARC-Kenya (4), FORD-Kenya (1), Ford-P (3), New Ford-K (2), Mazingira Party (1), Ford-A (1), DP (2) Wabunge wa kujitegemea waliingia kupitia vyama vidogo kama PDP (1), PPK (1), NLP (1), KADDU (1), UDM (1), PICK (1), CCU (1), Kenda (1) Nation 31-12-2007[dead link] Nation 09-01-2008 Archived 16 Januari 2008 at the Wayback Machine. |