BAKITA ni kifupi cha Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania.
BAKITA ni chombo cha serikali chini ya wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo.
Baraza hilo liliundwa na sheria ya bunge Na. 27 ya mwaka 1967 kwa shabaha ya kukuza, kuimarisha na kuendeleza Kiswahili hasa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika marekebisho ya sheria hiyo yaliyofanyika mwaka 1983 kwa Sheria ya Bunge Na. 7, BAKITA imepewa uwezo wa kufuatilia na kusaidia ukuzaji wa Kiswahili katika nchi za nje pia.
Pamoja na Chama cha Kiswahili cha Taifa (CHAKITA) cha Kenya na wawakilishi kutoka Uganda BAKITA imeunda Baraza la Kiswahili la Afrika Mashariki (BAKAMA).
Mwaka 2015 BAKITA ilifanikisha mradi wake wa kutunga kamusi mpya iliyoitwa Kamusi Kuu ya Kiswahili.[1]