Lanthani (Lanthanum) | |
---|---|
Jina la Elementi | Lanthani (Lanthanum) |
Alama | La |
Namba atomia | 57 |
Uzani atomia | 138.905 |
Valensi | 2, 8, 18, 18, 9, 2 |
Densiti | 6.126 g/cm3 |
Ugumu (Mohs) | 2.5 |
Kiwango cha kuyeyuka | 1193 K (920 °C) |
Kiwango cha kuchemka | 3737 K (3464 °C) |
Asilimia za ganda la dunia | 17 ppm |
Hali maada | mango |
Lanthani ni elementi ya kikemia yenye alama ya La. Namba atomia ni 57. Ni sehemu ya kundi la elementi za Lanthanidi ikihesabiwa kati ya ardhi adimu. Rangi yake ni kidhahabu - nyeupe, lakini hewani inapata haraka ganda la oksidi lenye rangi ya kijivu. Ni laini na inaweza kukatwa kwa kisu.
Jina linatokana na Kigiriki λανθάνειν lanthanein (kuficha) kwa sababu wanakemia walioitambua katika karne ya 19 waliona ugumu kuitenganisha na madini mengine.
Kuna matumizi ya lanthani katika teknolojia mbalimbali:
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Lanthani kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |