Namba atomia Elementi ya kikemia Alama Picha
57 Lanthani La
58 Ceri Ce
59 Praseodimi Pr
60 Neodimi Nd
61 Promethi Pm
62 Samari Sm
63 Europi Eu
64 Gadolini M-ngu
65 Terbi Tb
66 Disprosi Dy
67 Holmi Ho
68 Erbi Er
69 Thuli Tm
70 Ytebi Yb
71 Luteti Lu

Lanthanidi au lanthanoidi (Kiingereza: lanthanides au lanthanoids) ni kundi la elementi za kimetali zenye namba atomia kutoka 57 hadi 71, ambazo tabia zake zinafanana. Elementi hizo huhesabiwa kati ya madini adimu kama vile monaziti. Kundi hilo huanza na lanthani na kuishia kwa luteti. [1] [2]

Lanthanidi ni metali zinazofanana katika tabia nyingi. Nyingi hubadilika polepole kuwa hidroksidi zake wakati zimewekwa ndani ya maji, sawa na metali alikali.

Hewani huunda kwa kawaida ganda jembamba la oksidi wakati sawa na metali nyingi. Lanthanidi, pamoja na skandi na ytri, huhesabiwa kati ya elementi za ardhi adimu. Lanthanidi zote ni metali nyeupe na laini zinazobadilisha rangi ya nje haraka zikiathiriana na hewa. Ugumu wake huongezeka sambamba na namba atomia.

Lanthanidi hazipatikani wala hazichimbwi kwa viwango vikubwa.

Matumizi

Zina matumizi katika teknolojia mbalimbali kama vile:

Marejeo

  1. IUPAC Periodic Table
  2. IUPAC Periodic Table 2007 .pdf

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lanthanidi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.