Panama
Ramani ya Panama

Panama ni nchi ya mwisho kusini mwa Amerika ya Kati. Shingo ya nchi ya Panama hutazamwa kuwa mpaka kati ya bara la Amerika ya Kaskazini na lile la Amerika ya Kusini.

Imepakana na Kosta Rika na Kolombia; pwani ya Bahari ya Karibi iko upande wa kaskazini na pwani ya Pasifiki upande wa kusini.

Nchi iko kwenye sehemu nyembamba kabisa ya Amerika ya Kati.

Mfereji wa Panama hukata shingo la nchi na kufanya jina la Panama kujulikana kote duniani.

Historia

Baada ya ukoloni wa Hispania Panama ilikuwa sehemu ya kaskazini ya Kolombia. Majaribio mbalimbali ya uasi dhidi ya Kolombia kwa shabaha ya kuwa nchi ya pekee katika karne ya 19 hayakufaulu.

Mabadiliko makubwa yalikuja na ujenzi wa mfereji wa Panama.

Utangulizi wake ulikuwa reli kutoka Colon upande wa Karibi kwenda mji wa Panama upande wa Pasifiki iliyojengwa mwaka 1855. Reli hii ilirahisisha safari kati ya Atlantiki na Pasifiki kwa watu na bidhaa kuelekea Kalifornia. Watu wengi walikwenda Kalifornia miaka ile kwa sababu ya dhahabu iliyopatikana kule tangu mwaka 1848 na hapakuwa na reli kati ya pwani zote mbili za Marekani wakati ule.

Colon, Panama.

Wakati wa mwisho wa karne ya 19 Marekani ilianza kujenga mfereji kati ya bahari mbili wa kukata shingo la nchi. Serikali ya Marekani iliona umuhimu wa kutawala njia hii. Ikasaidia Wapanama waliotaka kujitenga na Kolombia kwa kutuma manowari Colon iliyozuia jitihada za Kolombia za kukandamiza ghasia hiyo.

Tarehe 3 Novemba 1903 Panama ilitangaza uhuru wake na kufanya mkataba na Marekani. Panama ilikodisha mlia wa nchi kwa pande zote mbili za mfereji kwa Marekani; Marekani iliahidi kutunza uhuru wa Panama.

Hali halisi ukanda wa mfereji ilikuwa eneo la Kimarekani hadi 31 Desemba 1999 iliporudishwa kwa serikali ya Panama.

Watu

Wakazi walio wengi (70%) ni machotara Waindio-Wazungu, 14% wana asili ya Afrika au ni machotara wa Kiafrika, 10% ni Wazungu na 6% Waindio.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kihispania.

Upande wa dini, 65-75% ni Wakatoliki na 15-25% Waprotestanti. Nje ya Ukristo, dini kubwa zaidi ni ile ya Bahai (2%).

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya ndani

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Panama
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika ya Kati bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Panama kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.