Papa Benedikto IX (1012 hivi – mwishoni mwa 1055 au Januari 1056) alipata kuwa Papa mara tatu: ya kwanza tangu Agosti/Septemba 1032 hadi Septemba 1044, ya pili tangu 10 Machi hadi 1 Mei 1045, na ya tatu tangu Oktoba 1047 hadi Agosti 1048[1].
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Theophylactus wa ukoo wa watawala wa Tusculum, Roma, Italia[2]..
Alimfuata mara ya kwanza Papa Yohane XIX, ya pili Papa Silvester III, na ya tatu Papa Klementi II.
Kila mara alifukuzwa madarakani kwa sababu ya matendo yake maovu[3] ila mara moja aliuza cheo chake, tendo la pekee kabisa katika historia ya Kanisa[4].
Hatimaye alifuatwa na Papa Damaso II[5].
![]() |
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Benedikto IX kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |